Hospital
ya Kumbukumbu ya Charles Kulwa Iliyopo katika Kata ya Uyovu Wilaya ya
Bukombe Mkoani Geita Imeendesha Zoezi la
upimaji wa magonjwa yasiyo yakuambukiza kwa watu wa jinsia zote wenye umri wa
kuanzia miaka hamsini na kuendele akizIndua kampeni hiyo Mkuu wa Wilaya hiyo
Said Nkumba alisema kuwa Upimaji huo umelenga kupima magonjwa
matatu ambayo ni Kisukari, Tezi dume pamoja na Shinikizo ladamu
(presha).
Akizungumza na wazee waliojitokeza katika zoezi hilo Mkuu huyo wa wilaya
alisema kuwa walichokifanya Hospital ya Kumbuklumbu ya Charles Kulwa ni kitendo
cha pekee na cha kuigwa kwa kwani magonjwa hayo yamekuwa ni mwiba mkali kwa
wazee hivyo wazee hao watapimwa bure na kisha kupatiwa huduma bure
“Niwapongeze kwa huduma hii mnaoitoa kwa jamii yetu kwani
mnafanya zoezi kubwa la huduma ya upimaji kwa wananchi kuweza
kupima magonjwa yasiyoambukiza wananchi wetu wa kata hii ya uyovu”
Alisema Mkuu wa Wilaya hiyo Nkumba


kushoto ni mkuu wa wilaya ya Bukombe Mhe,Said Nkumba akifanyiwa kipimo cha presha na nesi mmoja kati ya wafanyakazi wa Hospital ya Kumbukumbu ya Charles Kulwa Kwa upande wake
Said Lugeyo mmoja wa Wazee waliopatiwa huduma hiyo alisema kuwa anaipongeza
hospital ya kumbukumbu ya Charles Kulwa chini ya Mkurugenzi Mtendaji Dr. Baraka
Kulwa kwa jinsi ambavyo amekuwa msaada
mkubwa kwa jamii yetu ya Uyovu.
Aidha amemtaka
aendelee na moyo huo huo wa kuwathamini Wazee ambayo hawana kipato cha kuweza
kujitibia lakini ni wagonjwa.
“Anayoyafanya
kijana huyu Dr. Baraka yalikuwa yakifanywa miaka ya nyuma sana na marehemu
wazazi wake hivyo jambo hilo ni ishara kubwa kijana huyu amelelewa katika
misingi ya maadili mema yenye kuwathamini wazee” Alisema
Mmoja kati ya wazee waliojitokeza kupima akifanyiwa vipimo vya radiolojia
Naye Mkurugenzi wa Hospital ya Kumbukumbu ya Charles
Kulwa Dr. Baraka Kulwa ameeleza kuwa
Lengo la zoezi la Upimaji huo kutoa shukuru kwa Wazazi wake wote wa kata hiyo
ambao waliishi vizuri na waanzilishi wa hospital hiyo .
Aidha Dr. Baraka amewataka
wananchi wenye Umri wa kuanzia miaka 50 na kuendelea kujitokeza kwa wingi
kupima magonjwa hayo kwani yamekuwa ni tatizo kwa jamii kwa watua wenye umri
mkubwa,
pia alisema kuwa zoezi hili litakuwa ni endelevu kwa
kuwapima wazee na tunakusudia kufanya mara mbili kwa mwaka yaani mwanzo wa
mwaka na mwisho wa mwaka kwa kusudi la kuwasaidia wazee wetu kuweza kutambua
Afya zao.
Kulia ni Mkurugenzi wa Hospital ya kumbukumbu ya Charles Kulwa Akiteta jambo na Mkuu wa Wilaya ya Bukombe Mhe, Saidi Nkumba kabla ya uzinduzi ya magonjwa yasiyoambukiza
Mamia ya wananchi
waliojitokeza katika zoezi hilo la upimaji wakisubiri huduma
0 Comments:
Post a Comment